Gurudumu La Uchumi

Sehemu ya I: Mfumo mbovu au mafanikio, matajiri 4 Afrika kumiliki nusu ya mali za raia wa bara hilo

Informações:

Sinopsis

Katika bara lenye watu zaidi ya bilioni 1.4, ni watu wanne tu wanaomiliki utajiri zaidi ya nusu ya watu wote. Kulingana na ripoti mpya ya Oxfam, ukosefu huu wa usawa unaostua sio tu takwimu - ni ishara ya wazi ya ukosefu wa haki za kiuchumi uliokita mizizi, mifumo iliyovunjika na kukosekana kwa fursa. Kujadili haya yote nimewaalika Johnson Denge mtaalamu wa uchumi akiwa Nairobi na Apronius Mbilinyi yeye ni mtaalamu wa masuala ya Kodi akiwa Tanzania.