Mtazamo Wako Kwa Yaliyojiri Wiki Hii

  • Autor: Vários
  • Narrador: Vários
  • Editor: Podcast
  • Duración: 8:04:24
  • Mas informaciones

Informações:

Sinopsis

Makala yanayochambua masuala na matukio mbalimbali yaliyotokea kwenye jamii kwa wiki nzima kwa kina, yanatoa fursa kwa msikilizaji kueleza hisia na mtazamo wake juu ya masuala yanayoendelea kutokea iwe ni katika uga wa uchumi na siasa duniani kote.

Episodios

  • DRC:Rais Felix Tchisekedi awataka raia wa nchi yake kuunga mkono mabadiliko ya katiba

    30/11/2024 Duración: 19min

    Miongoni mwa yale utakayoyasikia kwenye habari ni pamoja na Rais wa DRC, Felix Tschisekedi, kuwataka raia wa nchi yake  kuunga mkono mabadiliko ya katiba, , Chama tawala cha CCM  nchini Tanzania chaongoza kwa asilimia 99 ya kura.Zaidi ya watu 100 hawajulikani walipo baada ya ajali ya maporomoko ya Udongo nchini Uganda,pia Tutaangazia ziara yake  Rais wa Nigeria, Bola Tinubu, nchini Ufaransa,  Raia wa Namibia wapiga kura,     kisha kimataifa tutaangazia mkutano wa  Mawaziri wa mambo ya nje kutoka muungano wa G7,uliofanyika mjini Roma Italia.

  • Maaskofu wa kikatoliki nchini Kenya wakosoa utawala, Rwanda yamaliza Marbug

    16/11/2024 Duración: 20min

    Maaskofu wa kanisa katoliki nchini Kenya wameukosoa utawala wa Ruto, wataka kukomeshwa, utekaji nyara na ukiukaji wa haki za binadamu, wapinzani nchini DRC wajitokeza kupinga mpango wa kubadilisha katiba, Rwanda yafanikiwa katika mapambano yake dhidi ya ugoinjwa wa Murbag, kura ya maoni kuhusu katiba mpya kufanyika jumamosi nchini Gabon,Kamati maalum ya Umoja wa Mataifa  yaunga mkono ripoti kwamba Israel inatekeleza mauaji ya kimbari jijini Gaza

  • Uchaguzi wa Marekani, mapigano DRC, kampeni za Raila kuwania uenyekiti wa tume ya AU

    09/11/2024 Duración: 20min

    Donald Trump achaguliwa kuwa rais wa 47 wa Marekani, Ziara ya rais wa Kenya William Ruto huko Addis Ababa Ethiopia, na Sudan Kusini, na Raila Odinga kuzindua azma yake ya kuwania uenyekiti wa tume ya Umoja wa Afrika, kuelekea uchaguzi huo utakaofanyika Februari mwaka 2025. Mapigano makali kati ya waasi wa M23 na wazalendo mashariki mwa DRC, Umoja wa Mataifa wasema uamuzi wa kuahirishwa uchaguzi nchini Sudani Kusini haukubaliki, Duma Boko atawazwa rasmi kama rais mpya wa Botswana, Uhusiano wa Urusi na Marekani baada ya Trump kushinda uchaguzi

  • Kithure Kindiki aapishwa kuwa makamu wa rais Kenya, ziara ya rais wa DRC nchini Uganda

    02/11/2024 Duración: 20min

    Kuapishwa kwa makamu mpya wa rais wa Kenya Profesa Kithure Kindiki, ziara ya rais wa DRC Félix Tshisekedi Kampala Uganda huku mapigano kati ya waasi wa M23 na wazalendo yakiripotiwa mashariki mwa nchi yake, mkutano wa Comesa watamatika Jijini Bujumbura Burundi, Umoja wa mataifa wasema hali ya kibinadamu nchini Sudan yatia wasiwasi, upinzani washinda uchaguzi mkuu Botswana, kampeni za lala salama Marekani, lakini pia kauli ya Korea Kaskazini kuwa itasimama na Urusi hadi ushindi wake huko Ukraine.

página 2 de 2