Siha Njema

  • Autor: Vários
  • Narrador: Vários
  • Editor: Podcast
  • Duración: 3:59:10
  • Mas informaciones

Informações:

Sinopsis

Makala inayojadili kwa kina masuala ya afya, tiba na kutambua magonjwa mbalimbali bila ya kusahau namna ya kukabiliana nayo. Watalaam walibobea kwenye sekta ya afya watakujuvya na kukuelimisha juu ya umuhimu wa kuwa na afya bora na si bora afya. Pia utawasikiliza kwa maneno yao watu ambao wameathirika na magonjwa mbalimbali na walikumbwa na nini hadi kufika hapo walipo.

Episodios

  • Ugonjwa wa Ukoma bado ni changamoto kubwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo

    29/01/2025 Duración: 09min

    DRC imeripoti maambukizi ya Ukoma mwisho wa mwaka jana na pia mwaka huu Ukoma ni ugonjwa unaoathiri sana ngozi na unaweza kuharibu baadhi ya viungo kama vile mikono ,miguu na hufanya mtu kutengwa na jamii

  • Ongezeko la mafua na magonjwa yenye dalili za mafua wakati wa joto

    21/01/2025 Duración: 09min

    Kumeendelea kushuhudiwa kwa idadi  kubwa ya watu wanaougua mafua au magonjwa yanayoathiri mfumu wa kupumua mwezi Januari ambao una joto jingi na vumbi.  Hii inajiri wakati China ikiwa imeripoti mlipuko wa ugonjwa wa Human metapneumovirus ,HPMV unaofanana na COVID 19 .Daktari  Juma Maleve kutoka Hospitali ya rufaa ya Mombasa ,Pwani ya Kenya anafafanua.

  • Dunia: Zaidi ya watu Milioni 18 wameathirika na ugonjwa wa mtindio wa ubongo

    07/01/2025 Duración: 10min

    Kwa kitaalam mtindio wa ubongo unaitwa Cerebral Palsy kwa kifupi CP..ugonjwa huu unatokana na jereha kwenye ubongo ambao huwa linafanya mtoto kushindwa kudhibiti misuli ya mwili wake hali inayoweza kusababisha viungo vya mtoto kulegea au kukamaa muda wote. Mtoto anaweza kupata majeraha kwenye ubongo akiwa bado yuko tumboni, wakati wa kuzaliwa au baadae maishani.CP husababisha ulemavu wa kudumu katika maisha yote ya mtoto.

  • Uzazi wa Mpango:Wanaume wajitolea kufanya upasuaji wa mirija -Vasektomia

    31/12/2024 Duración: 09min

    Vasectomy ni njia ya  kupanga uzazi ambayo  inahusisha upasuaji wa mshipa unaopitisha mbegu za kiume, ili mme asiweze kumpachika mke mimba. Ni njia ya upangaji uzazi ya milele.Na pengine unajiuliza hili linafanyiikaje na ina athari gani kwenyen afya ya mwanaume ?Sikiliza makala haya

página 2 de 2