Wimbi La Siasa

  • Autor: Vários
  • Narrador: Vários
  • Editor: Podcast
  • Duración: 4:02:13
  • Mas informaciones

Informações:

Sinopsis

Makala ya Wimbi la Siasa inakupa fursa ya kufahamu masuala ya kisiasa yanayoendelea ndani na nje ya Bara la Afrika. Kwenye Makala haya utapata habari ambazo zinakugusa moja kwa moja wewe msikilizaji. Kila wakati usikose kusikiliza Makala ya Wimbi la Siasa

Episodios

  • Tanzania: Mbowe na Lissu wakiweka CHADEMA njia panda

    08/01/2025 Duración: 10min

    Chama kikuu cha upinzani nchini Tanzania CHADEMA, kitawachagua vongozi wa ngazi ya juu wa chama hicho, Januari tarehe 21. Kibarua kigumu kipo kwenye ushindani wa nafasi ya Mwenyekiti.Freeman Mbowe ambaye amekuwa akiongoza chama hicho kwa zaidi ya miaka 20 na Makamu wake Tundu Lissu, ni miongoni mwa watia nia waliojitosa kupambania nafasi hiyo.Wawili hao wameendelea kutupiana maneno makali, na kuzua hofu kuhusu hatima ya chama hicho baada ya uchaguzi huo. Thomas Kibwana ni mchambuzi wa siasa za Tanzania, akiwa jijini Dar es salaam, anachambua kwa kina.

  • Msumbiji yaendelea kujipata kwenye mvutano wa kisiasa

    01/01/2025 Duración: 10min

    Heri ya mwaka mpya wa mwaka 2025. Nchi ya Msumbiji bado ipo kwenye mvutano mkali wa kisiasa, baada ya uchaguzi wa mwezi Oktoba mwaka 2024.Hali imeendelea kuwa mbaya baada ya Baraza la Katiba, kuthibitisha ushindi wa Daniel Chapo kutoka chama tawala FRELIMO, kuwa mshindi wa uchaguzi wa urais huku kiongozi wa upinzani Venancio Mondlane, akiendelea kudai aliibiwa kura.Watu zaidi ya 260 wamepoteza maisha, wengi wao wakipigwa risasi na polisi kwa mujibu wa mashirika ya kutetea haki za binadamu.

  • Hatua ya rais wa Kenya kuwateua wandani wa mtangulizi wake yazua maswali

    25/12/2024 Duración: 10min

    Makala ya wimbi imeangazia hatua ya rais wa Kenya, William Ruto, kuwajumuisha katika serikali yake mawaziri kadhaa waliohudumu wakati wa utawala wa mtangulizi wake Uhuru Kenyatta, na vile vile wandani wake kinara wa upinzani Raila Odinga., na hii ni licha ya yeye kuapa kutohusisha wapinzani kwenye Serikali yake; Ruben Lukumbuka anazungumza na Edwin Kegoli pia Torosterd Alenga ni wataalamu wa siasa za Kenya.

  • Kufeli kwa mkutano wa Luanda kwazua sintofahamu zaidi kwa usalama wa DRC

    18/12/2024 Duración: 10min

    Nini mustakabali wa eneo la mashariki ya DRC baada ya mkutano wa Luanda ambao uliitishwa na rais wa Angola kushindikana? Tarehe 15/12/2024 Rais Joao Laurenco wa Angola alikuwa amepanga kuwakutanisha marais wa DRC Félix Tshisekedi, na mwenzake wa Rwanda Paul Kagame, mkutano ambao haukufanyika kwa sababu rais wa Rwanda hakuridhia kushiriki. Ruben Lukumbuka anazungumza na John Banyene wa mashirika ya kiraia mkoani Kivu Kaskazini mashariki mwa DRC na Al Haji Abdulkarim Atiki mchambuzi wa siasa za kimataifa akiwa Daresalaam Tanzania.

página 2 de 2