Sinopsis
Jua Haki Zako ni makala yanayokuelimisha juu ya umuhimu wa kufahamu haki zako na sheria halali zilizomo kwenye jamii, mataifa na dunia kwa ujumla. Jua Haki Zako itakuelimisha juu ya masuala mbalimbali ya kisheria ndani ya Afrika Mashariki, Afrika na Duniani kwa ujumla.
Episodios
-
Serikali ya Uganda yapata shinikizo kumwachia kiongozi wa upinzaji Kizza Besigye
18/02/2025 Duración: 09minSerikali ya Uganda inapata shinikizo kutoka kwa wapinzani na watetezi wa haki za binadamu kumwachia huru mwanasiasa mkongwe Kizza Besigye anayekabiliwa na mashaka katika Mahakama ya kijeshi ambaye kwa siku kadhaa sasa amegoma kula akiwa gerezani, hali ambayo imedhoofisha afya yake.Tulimuuliza msikilizaji anazungumzia vipi masaibu yanayomkumba Besigye na anafikiri ni kwanini inachukua muda kuihamisha kesi ya mwanasiasa huyo kutoka Mahakama ya kijeshi kwenda kwenye Mahakama za kiraia ?
-
DRC : Haki ya raia wa Goma baada ya waasi wa M23 kuwasili eneo hilo
06/02/2025 Duración: 09minKatika makala haya tunazama kuangazia hali ya kibinadamu kule Goma baada ya waasi wa M23 kuwasili katika mji huo.Je hali ya kibinadamu ipo je baada ya waasi wa M23 kuwasili Goma. Kufahamu mengi zaidi skiza makala haya.
-
Africa : Serikali zinaendelea kukiuka haki za raia
28/01/2025 Duración: 10minShirika la kimataifa la kutetea haki za binadamu Human Right Watch limechapisha taarifa lituhumu serikali za Africa namna gani zimeshindwa kulinda haki za raia wake. Katika makala haya Benson Wakoli amezungumza na maafisa kutoka Human Right Watck kuelewa hali kamili/.Skiza makala haya kuelewa zaidi.
-
Juhudi zilizopo kuondoa hukumu ya kifo kwenye nchi barani Afrika
21/01/2025 Duración: 10minKatika nchi nyingi barani Afrika, adhabu ya kifo inasalia kuwa suala tata, ikiwa imejikita katika mifumo ya kisheria na kijamii. Licha ya mjadala kuhusu ufanisi na maadili yake kuendelea, wanaharakati wa haki za binadamu wanajitahidi kuhakikisha kufutwa kwa adhabu hiyo, wakisisitiza haki ya msingi ya kuishi. Ulaya tayari imeondoa adhabu ya kifo, ikitoa mfano wa mfumo wa haki unaolenga marekebisho badala ya adhabu kali.Kwenye makala haya tumeangazia juhudi hizo kuondoa adhabu hiyo .