Habari Rfi-ki

  • Autor: Vários
  • Narrador: Vários
  • Editor: Podcast
  • Duración: 3:57:56
  • Mas informaciones

Informações:

Sinopsis

Makala ya kila siku yanayompa fursa msikilizaji kutoa maoni yake juu ya habari zilizopewa uzito wa juu kwa siku husika. Msikilizaji hushiriki kwa kutuma ujumbe mfupi pamoja na kupiga simu.

Episodios

  • Nchini Kenya CAF yadhibiti idadi ya mashabiki viwanjani kwenye michezo ya chan

    12/08/2025 Duración: 10min

    Mada ya leo ni  kuhuus  michuano ya CHAN inapoendelea kushika kasi kwenye nchi za Kenya, Uganda na Tanzania, nchini Kenya baadhi ya mashabiki wamekuwa wakitumia nguvu kuingia uwanjani bila ya tiketi, hatua ambayo shirikisho la soka la Afrika CAF, limelazimika kupunguza idadi ya mashabiki kuingia uwanjani kwa sababu za kiusalama.,,tumemuuliza  nini kifanyike kudhibiti usalama wa mashabiki na viwanja? na Kwenye nchi yako wakati wa mechi kubwa hali huwaje?

  • Leo ikiwa ni siku ya ijumaa tarehe 08 08 2025 huwa ni mada huru .

    08/08/2025 Duración: 10min

    Leo ni siku ya mada huru. Tunampa nafasi mskilizaji kuchangia suala lolote ambalo limejiri nchini mwake wiki hii,na pia anaweza kuzungumzia kile ambacho amekisikia katika matangazo yetu ya juma hili.

  • Hatua ya wanasiasa kuhama hama vyama baada ya kukosa kufaulu kwenye uteuzi

    07/08/2025 Duración: 10min

    mada ya leo ni kuhusu Nchini Tanzania ambapo baadhi ya wanasiasa wa CCM ambao hawakufaulu katika uteuzi wa chama, wameanza kuhamia vyama vingine ili kugombea viti mbalimbali kwenye uchaguzi wa oktoba mwaka huu.Hali hii  imekuwa ikishuhudiwa pia katika mataifa mbalimbali barani Afrika. Tunamuuliza msikilizaji anaizungumziaje hatua hii ya hama hama kisiasa,na hali hii inashuhudiwa nchini mwake,,

  • Majadiliano ya Geneva kuhusu hatua za kukabiliana na matumizi ya plastiki

    06/08/2025 Duración: 10min

    Wawakilishi kutoka kote duniani wanakutana, wako Geneva, kujadili hatua za mwisho za kukabiliana na matumizi ya bidhaa za plastiki ambazo zimeendelea kuharibu mazingira.Tumemuuliza msikilizani ni njia zipi mbadala zitumike badala ya bidhaa za plastiki na anafikiri ni kwa nini nchi hazitaki kuachana na matumizi ya mifuko ya Plastiki.

  • Kwa nini biashara ya binadaam inazidi kushamiri licha ya hatari nyingi

    30/07/2025 Duración: 09min
  • Viongozi wakutana Ethiopia kujadili usalama wa njaa baa la njaa likishamiri

    29/07/2025 Duración: 09min
  • Msururu wa mashambulizi ya AL shabab nchini Somalia yanavyohujumu usalama

    29/07/2025 Duración: 08min

    Al Shabab imezidisha mashambulizi yake na kuiteka miji zaidi wakati vikosi vya umoja wa Afrika vikitarajiwa kuondoka

  • Maoni yako kwenye makala habari rafiki, mada huru

    25/07/2025 Duración: 09min
  • Tishio la kuzuka mzozo mpya kati ya Eritrea na Ethiopia kuhusu eneo la bahari

    22/07/2025 Duración: 09min

    Rais wa Eritrea Isaias Afwerki ameionya Ethiopia dhidi ya kuzuka tena kwa mzozo kwa kulazimisha kutumia eneo lake ya Bahari.

  • Afrika yaendelea kuathirika kufuatia hatua ya Marekani kusitisha misaada

    21/07/2025 Duración: 10min

    Nchini Zimbabwe wataalam wanasema wagonjwa wa Malaria wanaongezeka kwa kasi tangu Marekani kupitia shirika lake la USAID kukatisha misaada yake kwa nchi hiyo na bara la Afrika

  • Kenya yaondoa ulazima wa viza kwa mataifa ya Afrika isipokuwa Somalia na Libya

    18/07/2025 Duración: 10min
  • Wito wa mazungumzo ya kitaifa kutatua mizozo ya kisiasa Afrika

    17/07/2025 Duración: 10min
  • Marais wa Afrika kusalia madarakani kwa muda mrefu hata umri ukiwa umeenda

    15/07/2025 Duración: 09min
  • Viongozi wa Afrika watuhumiwa kuahidi mengi na kutimiza machache

    15/07/2025 Duración: 09min
  • Kila Ijuma unapata nafasi kuchangia chochote ndani ya rfi Kiswahili

    15/07/2025 Duración: 09min

    Kila Ijumaa rfi kiswahili inakupa nafasi ya kuchangia mada yoyote ile kwenye makala haya. Skiza maoni ya waskilizaji.

  • Kenya : Maandamano yatumika kupora mali

    15/07/2025 Duración: 09min

     Maandamano nchini Kenya na mataifa  mengine ya Afrika  yamekumbwa na mauaji na uporaji huku mali za watu zikiharibiwa. Je, unafikiri ni sahihi kwa waandamanaji kupora na kuharibu mali za watu? Nini vyombo vya usalama vinapaswa kufanya kuzuia uharibifu? Haya hapa baadhi ya maoni yako.

  • Viongozi wa Afrika wanatuhumiwa kuahidi mengi wakati wa kampeni na kutotimiza

    14/07/2025 Duración: 09min
  • Kenya: Mahakama ya juu yasema mwana haramu si haramu

    09/07/2025 Duración: 09min

    Katika makala haya tujadili hatua ya mahakama ya juu zaidi nchini Kenya, kuagiza kwamba mtoto aliyezaliwa nje ya ndoa kwenye dini ya kiislamu ana haki ya kumiliki mali ya babake kama watoto wengine waliozailiwa ndani ya ndoa, hatua inayoenda kinyume kabisa na tamaduni za dini hiyo. Unazungumziaje uamuzi huu wa mahakama nchini Kenya ? Haya hapa baadhi ya maoni yako.

  • Côte d'Ivoire : Kurejeshewa ngoma maalum kutoka Ufaransa

    08/07/2025 Duración: 09min

    Kaika makala haya tunajadili  hatua ya bunge nchini Ufaransa kupiga kura na kupitisha mswada wa kurudishwa nchini Ivory Coast ngoma maalum inayozungumza iliyochukuliwa katika nchi hiyo ya Afrika kutoka kabila la Ebrie wakati wa ukoloni mwaka 1916. Je umefika wakati kwa koloni za zamani za Bara la Afrika kurejesha vyombo walivyopora ?   Ndilo swali tumekuuliza . Haya hapa maoni yako.

  • Siku ya lugha ya kiswahili duniani makala maalum

    07/07/2025 Duración: 10min

    Siku ya kiswahili duniani, ambayo imekuwa ikiadhimishwa tangu mwaka 2022. Maadhimisho ya mwaka huu imefanyika jijini Kigali nchini Rwanda, ambako mamia ya wataalam na wapenzi wa Kiswahili wamekutana kwa siku mbili kujadiliana kuhusu nafasi na umuhimu wa lugha ya Kiswahili kwa raia wa nchi zote za Jumuiya. Kauli mbiu ni kusherehekea lugha ya Umoja, utambulisho na mchango wake kwa dunia.RFI kiswahili imeshirikiana na taasisi ya mafunzo ya biashara na ufundi stadi, NIBS ya jijini Nairobi, kuandaa makala maalum ya Habari RAFIKI na mwandishi wetu Ruben Lukumbuka ameongoza makala hii

página 1 de 2